Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

BELIEVE THE GOSPEL (IAMINI INJILI)

NAOMBA TWENDE PAMOJA KUHUBIRI INJILI. NA EV PETER KAMANIJA.

 
Baada ya Mungu kunipa maono ya kuhubili na kufundisha Duniani kote ikiwa ndio ujumbe mkuu kuwaambia watu ukweli wa injili nikawa sina jinsi zaidi ya kuanza  mipango na mikakati ya kuhakikisha alichonipa Bwana katika maono yake kinatimizwa kwa namna yoyote ile na kwa ghalama yoyote ili kufanikisha ujumbe huu wa Injili kuenea kwa hakikisho na utibitisho mkubwa wa Roho Mtakatifu. Kama Biblia isemavyo. utawezaje kutulia ikiwa BWANA amekupa agizo?” Yeremia 47:7.
Ndugu yangu  mpendwa katika Bwana tafadhali sana usomapo ufahamu kwamba Dunia yetu hii inamhitaji Mungu sana. Watu wanahamu kubwa ya kulisikia NENO LA MUNGU kuliko vile tunavyofikili. Hebu pata hamasa kubwa ya kuhakikisha ujumbe huu wa Kristo unahusika kwa kiasi kikubwa kuupeleka, tunawasema wazungu wanabarikiwa ni kwa sababu wako bize na kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu kwa namna yoyote wanayoweza. Mpendwa je si zaidi na kwangu Mimi na wewe tukijitoa kabisa kwa Mungu? Hakika Mungu hatakuacha atakubariki kwasababu umeugusa moyo wa Mungu.
Ndugu yangu mpendwa huduma hii ya Injili inahitaji  vitu vingi mno hakuna kitu utakacho kitoa kisiwe na kazi hata shilingi miamoja ina thamani kubwa mno. Tena usizalau.
Nimesema hivyo kwani huduma hii hasa niya vijijini, hebu angalia ndugu yangu  ni asilimia ngapi ya wahudumu wanao hubiri injili vijijini? Au wale wa vijijini wanatiwa moyo na akina nani? Tafadhali nyanyuka na mimi twende vijijini kuipeleka injili.
Siku moja mke wangu alimsikia mtu mmoja akisema katika kijiji furani toka nimefika hapa sijawahi kuona mkutano wa Injili”  kufuatilia kijiji hicho kwa mda wa huyo mtu ni miaka zaidi ya mitatu. Kwa mda huo Mijini imehubiliwa mikutano Mingapi? Moyo wangu unaniuma sana kiasi kwamba naona wakiniita “njoo na huku vijijini tunahitaji kuisikia injili”.
Moyo wangu unaripuka kwa moto mkuu, wa kuona vijiji vinakombolewa kwa Damu ya Yesu Kristo.
Mpendwa niwezeshe niipeleke Injili kisha taarifa nitakuwa naiweka wazi katika blog hii ili na wewe uone mambo ambayo mungu anafanya kupitia mkono wako wa kujitoa. Karibu tushiriki Baraka hii kwa pamoja.
Katika huduma hii ya vijijini sina namna, nawe ni shahidi maisha ya watu wanoishi huko vijijini yalivyo, ni duni mno, jamani ukiyaona hutatamani kwenda ukae huko. Lakini niwatu wa Mungu wale  wanahitaji injili kama inavyotakiwa pande zote duniani.
Ninatamani nikiwa naenda kwenye Injili vijijini huku nawapelekea misaada walau kidogo kwa kile ambacho watu wa Mungu mtakuwa mnanipa kukipeleka kwa watu hao.
Nia yangu, na moyo wangu ni Injili  iwashe moto mioyo ya watu wa vijijini. Mambo yanayofanyika vijijini ni aibu, watoto wanabakwa jamani, miaka mitatu, na kupanda, ndoa zinavunjika vibaya mno, hakuna amani zaidi ya majuto unajua ni kwanini?
Soma Rumi 1:28,  “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.”  Unaona lakini ukifuatilia juujuu utasema ndivyo ilivyo, nami nakuuliza swali fahamu zao zimefundishwa au kuuelekezwa na nani aliyejitoa kwenda kwao?
Mtu hawezi kukataa asichoambiwa, bali hukataa anachoambiwa je ndugu zetu hawa wameambiwa na nani mpaka wakatae au wakubali?
Soma kwa makini sura hii Rumi 10:13-15  “kwa kuwa, kila atakaye liitia jina la Bwana ataokoka”
Biblia iko wazi kabisa kila atakaye kuwa wazi kumuita bwana  ataokolewa. Swali ni hili naomba mimi na wewe tulijibu “basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije wasipoperekwa?...”  
shida sio kuhubiri, shida sio ujumbe shida ni muhubiri.
Nami leo nakataa kuwa shida sio Mhubili kwa sababu mimi nipo tayali kwenda shida ni hii NANI WA KUNIPELEKA HUKO?
Mpendwa nipereke ili tuishiriki baraka hii ya kristo. Unacho cha kupereka nami nimeereza kwenye mchanganuo wa mahitaji ya Injili kama ifuatavyo.

WATU
  • Waombaji
  • Watafiti wa maeneo ambayo hayajafikiwa ili tuyape kipaumbele kuyafikia.
  • Waimbaji
  • Wafuatiliaji baada ya watu kuokoka.
MALI NA FEDHA.
  •  Pesa tasilimu
  • Mali na vitu mbalimbali kama vile Nguo, viatu, chakula na chochote ambacho Mungu atkujalia.
VIFAA VYA INJILI
  • Vyombo vya injili kama generator, spika nk
  • Usafili kama gari, kutusafirisha, nk
  • Jukwaa la kutembea nalo
  • mahema ya pale tutakapo weka kambi. nk
Bwana Yesu  apewe sifa sana. mpendwa vitu ni vingi mno lakini kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Kama uko tayali. Kwa mawasiliano, ushauri, kujitoa naomba uwasiliane na mimi kwa
Namba zifuatazo
Ev Peter Kamanija
0757-537232
0787-537232








author
Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

NGOSHA
Powered by Blogger.

www.CodeNirvana.in

Pages

© Copyright BELIEVE THE GOSPEL
Back To Top