NAOMBA TWENDE PAMOJA KUHUBIRI INJILI. NA EV PETER KAMANIJA.

Baada ya Mungu kunipa maono ya kuhubili na kufundisha
Duniani kote ikiwa ndio ujumbe mkuu kuwaambia watu ukweli wa injili nikawa sina
jinsi zaidi ya kuanza mipango na
mikakati ya kuhakikisha alichonipa Bwana katika maono yake kinatimizwa kwa
namna yoyote ile na kwa ghalama yoyote ili kufanikisha ujumbe huu wa Injili
kuenea kwa hakikisho na utibitisho mkubwa wa Roho Mtakatifu. Kama Biblia
isemavyo. “utawezaje kutulia ikiwa BWANA
amekupa agizo?” Yeremia 47:7.
Ndugu yangu mpendwa
katika Bwana tafadhali sana usomapo ufahamu kwamba Dunia yetu hii inamhitaji
Mungu sana. Watu wanahamu kubwa ya kulisikia NENO LA MUNGU kuliko vile
tunavyofikili. Hebu pata hamasa kubwa ya kuhakikisha ujumbe huu wa Kristo
unahusika kwa kiasi kikubwa kuupeleka, tunawasema wazungu wanabarikiwa ni kwa
sababu wako bize na kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu kwa namna yoyote
wanayoweza. Mpendwa je si zaidi na kwangu Mimi na wewe tukijitoa kabisa kwa
Mungu? Hakika Mungu hatakuacha atakubariki kwasababu umeugusa moyo wa Mungu.
Ndugu yangu mpendwa huduma hii ya Injili inahitaji vitu vingi mno hakuna kitu utakacho kitoa
kisiwe na kazi hata shilingi miamoja ina thamani kubwa mno. Tena usizalau.
Nimesema hivyo kwani huduma hii hasa niya vijijini, hebu
angalia ndugu yangu ni asilimia ngapi ya
wahudumu wanao hubiri injili vijijini? Au wale wa vijijini wanatiwa moyo na
akina nani? Tafadhali nyanyuka na mimi twende vijijini kuipeleka injili.
Siku moja mke wangu alimsikia mtu mmoja akisema katika
kijiji furani “toka nimefika hapa
sijawahi kuona mkutano wa Injili”
kufuatilia kijiji hicho kwa mda wa huyo mtu ni miaka zaidi ya
mitatu. Kwa mda huo Mijini imehubiliwa mikutano Mingapi? Moyo wangu unaniuma
sana kiasi kwamba naona wakiniita “njoo na huku vijijini tunahitaji kuisikia injili”.
Moyo wangu unaripuka kwa moto mkuu, wa kuona vijiji
vinakombolewa kwa Damu ya Yesu Kristo.
Mpendwa niwezeshe niipeleke Injili kisha taarifa nitakuwa naiweka
wazi katika blog hii ili na wewe uone mambo ambayo mungu anafanya kupitia mkono
wako wa kujitoa. Karibu tushiriki Baraka hii kwa pamoja.
Katika huduma hii ya vijijini sina namna, nawe ni shahidi
maisha ya watu wanoishi huko vijijini yalivyo, ni duni mno, jamani ukiyaona
hutatamani kwenda ukae huko. Lakini niwatu wa Mungu wale wanahitaji injili kama inavyotakiwa pande
zote duniani.
Ninatamani nikiwa naenda kwenye Injili vijijini huku
nawapelekea misaada walau kidogo kwa kile ambacho watu wa Mungu mtakuwa mnanipa
kukipeleka kwa watu hao.
Nia yangu, na moyo wangu ni Injili iwashe moto mioyo ya watu wa vijijini. Mambo
yanayofanyika vijijini ni aibu, watoto wanabakwa jamani, miaka mitatu, na
kupanda, ndoa zinavunjika vibaya mno, hakuna amani zaidi ya majuto unajua ni
kwanini?
Soma Rumi 1:28,
“Na kama walivyokataa kuwa na Mungu
katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye
yasiyowapasa.” Unaona lakini ukifuatilia juujuu utasema
ndivyo ilivyo, nami nakuuliza swali fahamu zao zimefundishwa au kuuelekezwa na
nani aliyejitoa kwenda kwao?
Mtu hawezi kukataa asichoambiwa, bali hukataa anachoambiwa
je ndugu zetu hawa wameambiwa na nani mpaka wakatae au wakubali?
Soma kwa makini sura hii Rumi 10:13-15 “kwa kuwa,
kila atakaye liitia jina la Bwana ataokoka”
Biblia iko wazi kabisa kila atakaye kuwa wazi kumuita
bwana ataokolewa. Swali ni hili naomba
mimi na wewe tulijibu “basi wamwiteje yeye
wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo
mhubiri? Tena wahubirije wasipoperekwa?...”
shida sio kuhubiri, shida sio ujumbe shida ni muhubiri.
Nami leo nakataa kuwa shida sio Mhubili kwa sababu mimi nipo
tayali kwenda shida ni hii NANI WA KUNIPELEKA HUKO?
Mpendwa nipereke ili tuishiriki baraka hii ya kristo. Unacho
cha kupereka nami nimeereza kwenye mchanganuo wa mahitaji ya Injili kama ifuatavyo.
WATU
WATU
- Waombaji
- Watafiti wa maeneo ambayo hayajafikiwa ili tuyape kipaumbele kuyafikia.
- Waimbaji
- Wafuatiliaji baada ya watu kuokoka.
- Pesa tasilimu
- Mali na vitu mbalimbali kama vile Nguo, viatu, chakula na chochote ambacho Mungu atkujalia.
- Vyombo vya injili kama generator, spika nk
- Usafili kama gari, kutusafirisha, nk
- Jukwaa la kutembea nalo
- mahema ya pale tutakapo weka kambi. nk
Bwana Yesu apewe sifa
sana. mpendwa vitu ni vingi mno lakini kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Kama uko tayali. Kwa mawasiliano, ushauri, kujitoa naomba uwasiliane na
mimi kwa
Namba zifuatazo
Ev Peter Kamanija
0757-537232
0787-537232
Post a Comment